Thursday, 3 March 2016

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Nassor Ahmed Mazrui Ahojiwa na Jeshi la Polisi Zanzibar Na Kuachiwa Kwa Dhamana

By: Unknown On: 21:42
  • Share The Gag

  • Wakati polisi visiwani Zanzibar wakimhoji Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui jana, ulinzi uliimarishwa mjini Unguja huku askari wenye silaha na magari ya deraya wakifanya doria mitaani. 

    Mazrui, ambaye alifika makao makuu ya jeshi hilo saa 2:00 asubuhi akiambatana na wakili wake, ndiye aliyekuwa mkuu wa timu ya kampeni ya mgombea urais wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, katika uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba 2015, ambao chama chake kinaamini kuwa kilishinda.

    Barabara zinazoelekea makao makuu ya polisi kutokea Jang’ombe, Kilimani na Bomani zilifungwa huku vikosi vya ulinzi na usalama vikiwa vimetapakaa maeneo hayo na mitaa mbalimbali mjini Unguja.

    Wakazi wa Zanzibar wanaojiandaa kwa uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Machi 20, kuanzia Jumatano mchana walishuhudia askari wenye sare wakiwa katika magari maalumu ya kijeshi wakirandaranda kwenye barabara za Unguja, hususan mitaa ya Ng’ambo kupitia Mnazi Mmoja, Darajani, Amani, Chumbuni na Mtoni kuelekea Bububu.

    Wakati hali ikionekana hivyo mitaani, Mazrui alikuwa ndani ya Ofisi ya Upelelezi ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, Ziwani mjini Unguja ambamo alihojiwa kwa saa tatu na nusu.

    Alianza kuhojiwa tangu saa 2.00 asubuhi kama alivyotakiwa na jeshi hilo kuripoti kupitia barua ya wito aliyotumiwa hivi karibuni, hadi saa 5.30 

    Hata baada ya kumaliza kuhojiwa, Mazrui aliyekuwa waziri wa biashara, alilazimika kubaki kituoni hapo akisubiri kukamilika kwa taratibu za dhamana. Aliruhusiwa kuondoka saa 6.40 mchana.

    Pamoja na ulinzi kuimarishwa, mamia ya wananchi, hasa wapenzi, wanachama na wafuasi wa CUF, walifika makao makuu ya chama hicho yaliyoko Mtendeni ili kumpokea Mazrui akitokea polisi. 
     
    Baada ya kuachiwa kwa dhamana, Mazrui alisema alihojiwa na polisi kuhusu kauli aliyoitoa hivi karibuni alipokuwa Dunga Kiembeni, Wilaya ya Kati mkoani Kusini Unguja kwamba chama chake cha CUF kimechoshwa na vitendo vya hujuma na vya kihuni dhidi ya mali na ofisi zao.

    “Naam, nimewaambia kwamba hiyo ni kauli yangu na niliyesema hayo ni mimi kuwa CUF tumechoshwa na uhuni huo,” alisisitiza Mazrui mara baada ya kuachiwa kwa dhamana ya masharti ya kuwa na wadhamini wawili na kila mmoja wao kutakiwa kuweka hapo Sh500,000.

    “Wamesema nimetoa kauli za uchochezi hivyo watanishtaki mahakamani na wamenitaka niripoti polisi Jumanne na Alhamisi.” Alisema.
     
    Credit; Mpekuzi blog

    Apiga marufuku malori barabara za manispaa Dar

    By: Unknown On: 21:41
  • Share The Gag
  • Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik.

    MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amepiga marufuku utoaji wa vibali vya malori ya mizigo na magari yenye uzito wa zaidi ya tani 10 kuingia katika barabara zote zinazosimamiwa na Manispaa za jiji la Dar es Salaam.
    Barabara hizo ni zile zilizojengwa kwa kiwango cha lami na hatua hiyo inatokana na barabara hizo kuharibika kwa kipindi kifupi kutokana uzito jambo linaloisababishia Serikali hasara.
    “Kuanzia leo katika mkoa wangu ni marufuku kutoa vibali vya magari yenye uzito wa zaidi ya tani 10 kuingia kwenye barabara zetu, tunataka barabara zidumu, watakaokaidi watachukuliwa hatua,” alisisitiza Sadiki.
    Sadiki aliziagiza manispaa za jiji hilo kuweka alama za barabarani zinazoonesha zuio kwa magari yote yenye uzito wa zaidi ya tani 10 kupita kwenye barabara hizo ili wamiliki na madereva watakaokiuka agizo hilo wachukuliwe hatua kali za kisheria.
    Alikuwa akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Dar es Salaam kwenye kikao cha kwanza kwa mwaka 2016. Alisema manispaa za jiji hilo zinatenga fedha nyingi kujenga barabara mpya na kufanya matengenezo ya zilizopo lakini nyingi zinaharibiwa na malori ya mizigo.
    Alisema baadhi ya magari yenye uzito wa tani 40 hudiriki kupita kwenye barabara za huduma ama za dharura (service road), madaraja na wakati mwingine maeneo ya waenda kwa miguu na kusababisha uvunjaji wa kingo za barabara na milingoti ya taa za barabarani na kuongeza kuwa vitendo hivyo vinaisababishia Serikali hasara kutokana na gharama ya matengenezo.
    Kuhusu ulinzi na usalama wa watumiaji wa barabara za jiji hilo, ameitaka Polisi kuendelea kuchukua hatua na kufanya operesheni dhidi ya madereva wa pikipiki (bodaboda) na bajaji wanaopitisha vyombo vyao vya usafiri kwenye njia za waenda kwa miguu na kusababisha usumbufu na ajali za mara kwa mara.
    ‘‘Ninaiagiza manispaa ya Kinondoni kuondoa wafanyabiashara wote walioko eneo la kituo cha kuzalishia umeme Ubungo, eneo lile ni hatari kwa usalama na maisha yao, kukaa pale ni kinyume cha sheria,’’ alisema Sadiki.
    Alisema mwaka huu Mkoa wa Dar es Salaam umetenga Sh bilioni 343.5 ikilinganishwa na Sh bilioni 266.6 zilizotengwa mwaka 2015/2016 kutekeleza ujenzi na matengenezo ya barabara katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo ili kupunguza msongamano wa magari.

    Chanzo HabariLeo.


    Mganga, mwanafunzi mbaroni kwa utoaji mimba

    By: Unknown On: 21:38
  • Share The Gag

  • Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Mihayo Msikhela

    MGANGA wa tiba za asili, Juma Ramadhani pamoja na mwanafunzi wa Chuo cha Utalii Masai, Saumu Mohamed (19) wanashikiliwa na Polisi mkoani Tanga kwa tuhuma za kuharibu mimba ya miezi saba.
    Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Mihayo Msikhela aliwaambia waandishi wa habari jana, watuhumiwa hao ambao ni wakazi wa mtaa wa Sahare, walikamatwa Februari 29 mwaka huu saa 2:00 usiku katika mtaa huo ulio kata ya Mzingani.
    Alisema kukamatwa kwao kumekuja baada ya wananchi kuokota maiti ya mtoto mchanga mwenye jinsia ya kike ambaye inadaiwa alikuwa ni mimba ya miezi saba.
    “Siku hiyo ya tukio katika maeneo ya Sahare jijini Tanga aliokotwa mtoto wa kike ambaye ni mimba ya miezi saba. Inadaiwa mimba hiyo iliharibiwa na Saumu ambaye in mwanafunzi wa Chuo cha Utalii Masai cha mkoani hapa”.
    Alisema na kuongeza: “Binti huyo kulingana na uchunguzi wetu wa awali anadaiwa kunywa dawa ya kutoa mimba kwa kutumia dawa maalumu ambayo alipewa na mganga wa kienyeji aitwaye Juma Ramadhani na ndipo ikaharibu ujauzito huo na kisha Saumu alipofanikiwa kujifungua, akaamua kutupa maiti ya mtoto huyo ambayo baadaye iliokotwa na wananchi.”
    Alisema watuhumiwa wote wanashikiliwa na Polisi na watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

    Chazo HabariLeo.

    Naibu Waziri wa Afya Dr Kigwangala Azindua Wodi Mpya Ya Wagonjwa Mahututi Muhimbili.....Kasema Serikali ina Mpango wa Kuacha Kupeleka Wagonjwa Nje ya Nchi Kutibiwa

    By: Unknown On: 21:31
  • Share The Gag
  • Serikali imesema ina mpango wa kusitisha kupeleka wagonjwa nje ya nchi kupatiwa matibabu na kuhakikisha kila kitengo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kinakuwa na chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU).

    Serikali imechukua uamuzi huo, wakati taarifa ndani ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto zikieleza inadaiwa deni la Sh.28.74 bilioni za malimbikizo kutokana na ongezeko la wagonjwa wanaopelekwa nje kwa matibabu.

    Akizungumza jana wakati wa kuzindua chumba cha ICU kilichopo jengo la Mwaisela hospitalini hapo, Naibu Waziri wa wizara hiyo, Dk Hamis Kigwangalla alisema lengo la Serikali ni kuanzisha vyumba hivyo kwa kila kitengo ili kupunguza vifo.

    Alisema hospitali hiyo ina vitanda 25 vya ICU, lakini lengo ni kuwa na vitanda 150 vya wagonjwa mahututi na wataalamu wa kutosha.

    Alisema Serikali ina mpango wa kutoa mafunzo kwa madaktari na wauguzi watakaokuwa wamebobea katika fani ya vyumba hivyo.

    Madaktari na wauguzi hao watapata mafunzo kutoka Chuo Kikuu cha Cairo na mengine yatatolewa kupitia Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (Muhas).

    Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Lawrence Mseru alisema kuzinduliwa kwa ICU hiyo kunaifanya hospitali hiyo kuwa na vyumba vya aina hiyo viwili vyenye vitanda 25, kutoka chumba cha awali kilichokuwa na vitanda vinane.

    Alisema uwapo wa vitanda hivyo ni ongezeko la asilimia 200 ikilinganishwa na uwezo wa awali.

    “Fedha za ndani zilizotumika kwa ajili ya ukarabati wa chumba hiki ni Sh230 milioni ikiwa ni pamoja na kutafuta ufadhili kutoka taasisi isiyo ya kiserikali ya Ujerumani iliyowekeza vifaatiba vya Sh600 milioni.

    ‘‘Mfadhili huyu ndiye aliyetununulia vifaa vyenye thamani ya Dola 800,000 za Marekani,” alisema Profesa Mseru. 
    Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akisisitiza jambo jana Jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi ya wodi ya ICU ilizopo kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH)
    Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hosptitali ya Taifa ya Muhimbili MNH, Profesa Lawrence  Museru (katikati) akitoa maelezo mafupi jana Jijini Dar es Salaam kwa  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya  Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla (kulia) wakati wa sherehe za uzinduzi wa wodi ya ICU iliyopo kwenye jengo la Mwaisela katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH)
    Rais wa Shirika lisilo la Kiserikali la Madaktari wanaohusika na magonjwa ya ini na tumbo(Gastrenterology) kutoka Munich Ujerumani(kulia) akiteta jambo na  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya  Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati wa uzinduzi wa ICU Muhimbili.
     
    Credit; Mpekuzi blog

    Marais EAC waimba ‘Hapa Kazi Tu’

    By: Unknown On: 21:26
  • Share The Gag
  • MARAIS wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wameanza kuzungumza lugha moja wakisisitizana kuchapa kazi, kuondokana migogoro ya ndani na porojo za kisiasa kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.
    Msimamo wa viongozi hao ulijidhihirisha jana kupitia hotuba zao kwenye hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara yenye kilometa 234.3 kutoka Arusha-Holili hadi kuingia Voi, Kenya itakayogharimu dola za Marekani milioni 353. Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na marais Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyatta wa Kenya na James Wani Igga aliyemwakilisha Rais wa Sudan Kusini, Salva Kirk.
    Wakiongozwa na mwenyeji wao, Rais John Magufuli, anayeongozwa na falsafa ya ‘Hapa Kazi Tu’ katika kuongoza Tanzania, marais Uhuru na Museveni walidhihirisha utayari wao wa kuunga mkono falsafa hiyo, kuhakikisha wanazifikisha nchi wanachama kwenye neema.
    Katika hotuba yake, Magufuli aliwataka marais wenzake kujikita katika kushirikiana na kuacha tofauti za ndani kwa kuwa wananchi wanasubiri maendeleo kwa kasi ya hali ya juu. Akihimiza nchi wanachama kumaliza tofauti za ndani mwao, Magufuli alisema nchi za EAC ni tajiri ingawa kwa sasa ni masikini wa kutupwa na ombaomba.
    Alisema hazipaswi kuwa ombaomba, bali kinachotakiwa ni kujipanga kikamilifu na kusonga mbele na kuacha tofauti ya kiitikadi ndani ya vyama vya siasa uchaguzi ulishapita. Alisisitiza kwamba wananchi wa EAC wana shida nyingi. “Hatutakiwi kuwa masikini kiasi hiki. Ni lazima tufike mahali tujiulize ni nani aliyeturoga, kama yupo mchawi lazima tumtafute tumkemee...,” alisema.
    Malizeni matatizo ndani
    Magufuli alisema kila nchi ina matatizo yake ya ndani, ambayo yanapaswa kutatuliwa kuhakikisha rasilimali zake zinatumika kuleta maendeleo. Alitoa mfano wa Sudan Kusini yenye madini aina zaidi ya 22, eneo la kilimo na ng’ombe wengi, kwamba wanakabiliwa a mgogoro wa kugombania madaraka ambao hawana budi kuumaliza na kusonga mbele.
    “Hata Tanzania tunayo matatizo yetu, hata Rwanda wana matatizo yao… Kwa sisi tuliopewa dhamana, tushiriki kikamilifu kuondoa matatizo ya nchi zetu,” alisisitiza. Aliendelea, ‘’Sasa umefika wakati sisi viongozi (marais) kumaliza matatizo ya ndani ya nchi na nchi kusonga mbele kwani ni viongozi wa wananchi wa itikadi zote,dini zote na makabila yote bila ya kubagua’’.
    Rais Magufuli alisema yeye akiwa Mwenyekiti wa EAC, wameamua kwa pamoja kujenga viwanda katika nchi hizo kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi zao, kwani kwa sasa asilimia 63 ya vijana hawana ajira.
    Alisema marais wa EAC wameamua kujenga viwanda kwa lengo la kutoa ajira kwa vijana hao, ambao wako vijiweni na hiyo itasaidia mazao ya kilimo na biashara yanayolimwa katika nchi hizo, kupata soko na kuuzwa ndani ya ukanda na hata nje kwa faida ya wananchi.
    Rais alieleza kusikitishwa kuona zao la biashara kama vile pamba, inalimwa nchini lakini inasafirishwa kwenda nje na kutengenezwa nguo na baadaye zinarudishwa nchini kama mitumba baada ya kuvaliwa. Alisema Tanzania sasa haiwezi tena kuwa shamba la bibi kwa wachache kujinufaisha zaidi na masikini kuwa masikini zaidi.
    Utumbuaji majipu bado
    Rais alisema uamuzi anaofanya wa kuwachukulia hatua watu wanaotumia vibaya madaraka na wala rushwa, si wa kuwaonea, bali vipo vitu vya hovyo ambavyo vimefanyika na kuumiza mamilioni ya Watanzania. Alisisitiza kwamba, wote waliofanya hivyo watachukuliwa hatua na kufikishwa mahakamani, hatimaye wafungwe.
    ‘’Nisipochukua hatua kwa mambo yalivyofanyika, haina haja ya mie kuwa Rais. Kuna mambo ya hovyo hovyo jamani yamefanyika. Nitawafukuza tu. Hilo halina msamaha,’’ alisema. Magufuli aliomba wananchi wa EAC wawe watulivu, akisisitiza kwamba marais wameamua na ndiyo maana miongoni mwa maazimio yao ni kufanya nchi ziwe na viwanda.
    Alisema viongozi wakiungwa mkono na wakaombewa kwa Mungu, wataweza kutekeleza waliyodhamiria. “Mkituombea tutekeleze tunayoweza kufanya tutaweza, msipotusaidia hatutaweza… na ndiyo maana kwa Watanzania wenzangu tumekuwa na hatua ndogo ndogo tunazofanya kushughulikia watu walioneemeka na mambo ya hovyo.
    Alisema kwa upande wa Tanzania, kazi ya kutumbua majipu inaendelea na hata idadi ikifika 2,000 haoni tatizo, ilimradi Watanzania walio wengi wanufaike. “Watuache tufanye kazi kwa ajili ya Watanzania walio wanyonge. Tanzania ilikuwa shamba la bibi, watu walikuwa wakifanya ya hovyo. Nimekuwa waziri kwa miaka 20 ninayajua,” alisema.
    Alisisitiza kwamba mambo ya mateso kwa wananchi hayana chama. Alisema hatua wanazotaka kuchukua ni kwa ajili ya maslahi ya wananchi wote bila kujali itikadi zao. Huku akikiri kwamba kazi hiyo ni ngumu na ya ajabu, aliendelea kuomba waombewe lengo la kusaidia wananchi litimie.
    “Tusipofanya, hakuna sababu ya mimi kuwa rais, ni vyema niende nyumbani nikalale, hakuna sababu ya mimi kuitiwa rais..kwa hiyo nawaomba ndugu zangu Watanzania mniunge mkono tufanye haya tunayofanya….mambo ya hovyo.” Aliendelea kusema, “ juzi tumeshindwa kuingia mambo ya roaming kwenye EAC kwa sababu sisi hatujasafisha nyumba yetu.
    Kwenye TCRA ilibidi nifukuze baadhi ya wafanyakazi ; Pale zaidi ya Shilingi bilioni 400 zimepotea, tungeweza kununua ndege na kutengeneza barabara. Lakini watu wamechezea pale na bado wanajiita wasomi.
    Na ndiyo maana tumeamua kufukuza, na tutawafukuza na bado watapelekwa mahakamani. Wafungwe wapate machungu ya wananchi waliyotengeneza miaka mingi,” alisema akisisitiza kuwa ni lazima ifike mahali waache kuvumiliana na kuoneana aibu.
    Aonya uvyama
    Magufuli ambaye alitumia nafasi hiyo, kuwashukuru wakazi wa Arusha kwa kumchagua kuwa Rais, aliwahakikishia kuwa yeye ni Rais wa Watanzania wote akisisitiza kutowabagua kwa misingi ya vyama na itikadi nyingine.
    “Nataka niwahakikishie mimi ni kazi tu,” alisema. Alimpongeza Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari akisema hana makeke, anajali maisha ya watu. “Nisipompongeza nitakuwa mnafiki.
    Ni kijana safi, hana makeke, anajali maisha ya watu…uchaguzi umeisha, tufanye kazi tuhakikishe wananchi wanapata maendeleo,” alisema na kutania akisema, “Ukimuona Nassari sura yake ni Chadema lakini moyo wake ni CCM.”
    Aliwaambia marais wenzake kwamba, wananchi wote walio kwenye nchi za jumuiya wanachohitaji si vyama, bali wanataka maisha mazuri. Alisema mambo ya kuomba omba misaada hayana budi kuisha.
    Vile vile alisema mambo ya watu wachache kuwa matajiri na wengine wakabaki masikini , pia yaishe. Alisema marais wa nchi wanachama wanapaswa kujikita kubadilisha maisha ya wananchi wote wa Afrika Mashariki.
    Uhuru afagilia ‘Kazi Tu’
    Kwa upande wake, Rais wa Kenya, Uhuru alisema, “Tupunguze maneno na sasa iwe kazi tu wananchi wafurahie nchi zao. Tutengeneze kila kitu hapa hapa EAC na siyo kununua kutoka nje ya nchi hii ni aibu.”
    “Tunapaswa kuanza rasmi safari ya kwenda Kanani (matumaini) na safari hii ndefu sana, lakini ina manufaa kwa wananchi wa nchi za EAC kwani safari hiyo ikikamilika na kufika kunakohitajika, vijana wengi watapata ajira,” alisema.
    Aidha, alisema anatambua historia ya Rais Magufuli akiwa Waziri jinsi alivyowezesha ujenzi wa barabara nchini. Alimwomba aendelee na ujenzi wa barabara ziungane na nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
    Akihimiza uchapa kazi, Uhuru alisema serikali za nchi za EAC zimelala na siyo wananchi kwani wanashirikiana kwa kila hali ikiwemo kufanya biashara kwa pamoja bila ya kubaguana. Rais Uhuru alisema wananchi wa EAC wanafanya biashara kila mara na kila kona lakini viongozi wa nchi hizo wako katika usingizi mzito kwa kuweka vikwazo vya hapa na pale.
    Alisisitiza marais kuondoa vikwazo hususan mipaka na vizingiti , badala yake waruhusu wananchi wafanye biashara ya wazi bila ya kificho kwa maslahi ya nchi hizo za ukanda. Alisema viwanda vingi vya nguo vimekufa katika nchi za jumuiya bila sababu za msingi.
    “Na sasa tunaamua kuvaa mitumba. Hilo lazima libadilike,” alisema. Aliendelea kusisitiza, “mmejaliwa kuwa na gesi na gesi iwanufaishe kwa asilimia kubwa na pia gesi hiyo ije nchini kwangu kwa kuuzwa kwa bei nafuu.”
    Museveni ‘akubali’ Rais Yoweri Museveni wa Uganda alisema Afrika imelala, inashtuka kutaka maendeleo wakati kumekucha, jambo alilosema kwa sasa halitakiwi kwa watu wa EAC, kwani wanapaswa kuamka na kufanya kazi ya kuinua uchumi bila ya woga.
    Rais Museveni alisema serikali ya Tanzania imejitahidi kujenga barabara zake za ndani, tofauti na zamani hivyo nguvu hiyo inapaswa kuunganishwa katika nchi za jumuiya. Alisema zamani alikuwa akitumia gari aina ya Land Rover ya kizamani kusafiri katika baadhi ya mikoa lakini kote huko kulikuwa hakuna lami bali kulikuwa na vumbi.
    Alisema lakini sasa anaweza kuja nchini na usafiri huo hadi jijini Dar es Salaam kwa kuwa kila kona kuna lami. Aliomba viongozi wenzake kushirikiana kwa dhati kujenga barabara katika nchi za EAC akisisitiza kuwa hizo ni sehemu ya shughuli za kimaendeleo na kiuchumi zitakazowezesha nchi kusonga mbele bila vikwazo.
    Barabara iliyozinduliwa Mradi huo wa ujenzi wa barabara unagharimiwa na Shirika la Jica la Japan, Benki ya Afrika (ADB) pamoja na fedha za Serikali ya Tanzania. Rais Magufuli alisema, kwa mara ya kwanza Arusha itakuwa na barabara yenye njia nne.
    Licha ya marais Museveni, Kenyatta wakiwa na mwenyeji wao Rais Magufuli, viongozi wengine waliohudhuriwa sherehe hizo za kuweka jiwe la msingi, ni pamoja na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein na viongozi wa EAC akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya aliyemaliza muda wake, Dk Richard Sezibera.

    Chanzo HabariLeo.

    Makundi ya kihalifu yameibuka - Polisi

    By: Unknown On: 21:25
  • Share The Gag

  • Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Ernest Mangu akimuapisha Kamishna wa Polisi, CP Nsato Marijani baada ya kupandishwa cheo na Rais.

    POLISI imesema ina taarifa juu ya kuibuka kwa makundi ya kihalifu nchini na imejipanga kukabili wahusika. Aidha, Kamishna Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Nsato Marijani, amehadharisha askari na watendaji wa jeshi hilo, aliowataja kuwa wasaliti na kusema watakaobainika watafukuzwa na si kuhamishwa vituo.
    Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuhusu mikakati ya jeshi katika mapambano ya uhalifu nchini, Marijani amewataka wananchi kuwa watulivu , kutotaharuki kwa kile alichosisitiza kuwa nchi iko salama wakati Polisi ikiendelea kujipanga kukabili vikundi husika.
    Kamishna Marijani alisema makundi ya uhalifu yanayoibuka nchini yamekuwa kero . Alisema juhudi za makusudi zinafanywa kuyadhibiti kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama.
    “Hatuwezi kuweka mikakati yetu hadharani ya kukabiliana na vikundi vya uhalifu vilivyoibuka hivi sasa, ila wafahamu kwamba tutawadhibiti kikamilifu,” alisema Kamishna Marijani. Alisema hakuna haja ya wananchi kuwa na hofu bali wawe watulivu na kuendelea kufanya shughuli zao za uzalishaji mali, kwa sababu vyombo vya usalama vipo na vitahakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unalindwa .
    Alisisitiza kwamba, ni vyema kwa raia wanapoona tabia au mienendo yenye mashaka ya watu, watoe taarifa Polisi. Polisi wasaliti Akizungumzia suala la nidhamu kwa askari na watendaji wa jeshi hilo, Kamishna Marijani alisema watendaji wengi wa jeshi hilo wana nidhamu na wanafanya kazi kwa weledi.
    Hata hivyo, alisema wapo wachache wanaochafua jeshi hilo. Alisema watakapobainika, hawatawavumilia wala kuwahamisha vituo vya kazi, bali watafukuzwa. “Watendaji wetu wengi wana nidhamu, ila wapo wachache wanaotuchafua, kuanzia sasa hatutawahamisha vituo vya kazi, tutawafukuza, kama walizoea huko nyuma , sio zama hizi, wajue kila zama zina vitabu vyake”, alisisitiza .
    Alisema hatua hiyo wataitekeleza bila uoga wala kificho . Aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo kuhusu taarifa za watumishi wa jeshi hilo wasio na maadili ili hatua zichukuliwe.
    Hivi karibuni, kumejitokeza matukio kadhaa ya uhalifu hususan jijini Dar es Salaam. Miongoni mwa matukio hayo, ni uvamizi wa benki ya DCB katika eneo la Chanika, wilayani Ilala. Uvamizi mwingine ulifanyika Benki ya Access , Tawi la Mbagala.

    Chanzo HabariLeo.

    Majaliwa: Tanzania itajitegemea kwa 80% katika bajeti

    By: Unknown On: 21:21
  • Share The Gag
  • Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akionesha usinga na mkuki ambavyo alipewa na wazee wa Kisukuma wa Busega katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Lamadi, juzi. Wazee hao pia walimbatiza jina la Massanja.

    WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa alisema Tanzania inaweza kujitegemea kwa zaidi ya asilimia 80 katika bajeti yake kutokana na vyanzo vyake vya ndani. Amesema kutokana na rasilimali zilizopo, Tanzania inaweza kukidhi bajeti yake kwa asilimia 80 bila kutegemea msaada kutoka nje na kwamba suala la kukabiliana na ufisadi na ukwepaji kodi ni endelevu.
    Waziri Mkuu Majaliwa alisema hayo juzi mjini Lamadi wakati akihutubia maelfu ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika siku ya kwanza ya ziara yake ya siku sita mkoani Simiyu. “Tanzania inaweza kujitegemea kwa asilimia 80 kwa mapato yake kutokana na rasilimali na vyanzo vyake vya ndani.
    Hili linawezekana. Ndio maana tumeamua kubanana,” alieleza Waziri Mkuu. Alisema ndio maana wameamua kupambana na ufisadi na ukwepaji kodi kwa nia ya kuhakikisha wanapata fedha za kuwatumikia Watanzania kwa fedha za ndani kupitia mapato yake.
    Alisema hata uamuzi wa kupitisha fedha zote katika Mfuko Mkuu wa Serikali ulikuwa na nia ya kutambua mapato yake yote ili fedha hizo zikasaidie kuleta maendeleo ikiwamo kuisimamia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kubana mianya yote ya ukwepaji kodi.
    Alisema hali hiyo imesaidia kwani mapato yameongezeka kutoka Sh bilioni 1.3 Desemba mwaka jana, Sh bilioni 1.5 Januari mwaka huu na mwezi uliopita, alisema ana hakika zitavuka zaidi.
    Alisema kutokana na hali hiyo, serikali ndio maana inagharimia mambo yake mengi likiwamo suala la elimu bure, na kwamba licha ya kuwapo kwa changamoto mbalimbali, watahakikisha Watanzania wanapata huduma mbalimbali zilizoboreshwa.
    Aliyekuwa Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum akiwasilisha bungeni mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2015/16, Juni mwaka jana, alisema jitihada za kuongeza mapato zimelenga kuisaidia Serikali kupunguza utegemezi wa bajeti ya Serikali kwa fedha za wahisani.
    Alisema kiwango cha utegemezi kimepungua kutoka asilimia 24 mwaka 2004/05 hadi asilimia 17 mwaka 2010/11. Alisema pia kwamba utegemezi huo umekuwa ukipungua mwaka hadi mwaka. Mwaka 2015/16 ilitarajiwa upungue kwa asilimia 6.4.
    Kuhusu suala la mipaka kati ya hifadhi na vijiji, Waziri Mkuu alisema amekwishaagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kusimamia suala hilo na kuhakikisha wanaliangalia limalizike kwa busara.
    Lakini ameagiza wananchi hasa katika wilaya za Busega na Bariadi kutoingia tena katika hifadhi ambako inadaiwa wanapokonywa ng’ombe wao na askari wa Wanyamapori kwa kutozwa Sh milioni tano hadi 10.
    Amewaonya askari hao wa Wanyamapori kuacha tabia hiyo na kwamba mwananchi yeyote mwenye taarifa za askari anayeshiriki vitendo hivyo, kupeleka jina lake kwa vyombo husika.

    Chanzo HabariLeo.