Monday, 16 November 2015

Tagged Under:

Samia ataka nchi kuzidi kuombewa

By: Unknown On: 23:24
  • Share The Gag
  • Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samiah Hassan Suluhu akisalimiana na viongozi wa dini.

    MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania ina utajiri mkubwa unaoangaliwa na watu wa mataifa mbalimbali hivyo kuwaomba viongozi wa dini kuwaombea ili wapate viongozi watakaouangalia utajiri wa Tanzania kwa ajili ya Watanzania wenyewe.
    Aliyasema hayo jana wakati akizungumza na viongozi wa dini kwa ajili ya kuwashukuru kwa maombi yao ya kuliombea Taifa wakati wa uchaguzi ili ufanyike kwa amani na utulivu. Alisema viongozi wa dini waendelee kuwaombea ili nchi zinazotaka kuigombanisha ili zitumie utajiri wa Tanzania kujinufaisha, zisipate nafasi na hilo litawezekana kwa kupata viongozi bora.
    “Tanzania ni kwa ajili ya Watanzania, nimeshuhudia katika kampeni mgodi wa Geita ukiwa na dhahabu ya kutosha lakini vijiji vya jirani ni maskini wa kutupa. Wanaozunguka wanahangaika na kituo cha afya tu kwa ajili ya afya zao, tuna kazi kubwa ya kufanya,” alisema.
    Kwa upande wake, Mwakilishi wa PCT, Askofu Yohana Masinga aliiomba Serikali ya Awamu ya Tano kuongeza ulinzi na usalama wa raia kwani katika awamu iliyopita kulikuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani kwa makanisa kuchomwa moto. Naye Kaimu Shekhe wa Mkoa wa Dodoma, Ahmed Said alimshukuru Mungu kwa kuuvusha uchaguzi kwa amani na utulivu.

    Created by Gazeti la HabariLeo.

    0 comments:

    Post a Comment